LOGO

LOGO

Saturday 31 January 2015

Miji mikongwe zaidi duniani!

Kadri idadi ya watu inavyoongezeka duniani, kwa baadhi ya nchi hulazimu kuunda mikoa mipya au miji mipya ili kuendana na kasi ya ukuaji huo kwa ajili ya kurahisisha huduma mbalimbali za jamii. Lakini nenda uendako, idadi ya watu itaongezeka na miji itaongezeka lakini miji ifuatayo itabaki kuwa miji mikongwe zaidi duniani.



1.Damascus,Syria.
Ni mji mkuu wa nchi ya Syria ambao pia ndio mji mkubwa zaidi kijiografia nchini humo. Unakadiriwa kuwa na population ya watu zaidi ya milioni 4.5. Mji huu unakadiriwa kuwepo tokea kipindi cha kati ya miaka ya 10,000-8,000 B.C, hivyo kuufanya kuwa mji mkongwe zaidi duniani.

Mji huu pia ndio kiungo muhimu zaidi cha nchi ya Syria kwani ndio moyo wa shughuli zake zote za iutawala, kibiashara na kitamaduni.

Vivutio vikubwa vinavyofanya watalii kumiminika katika mji huu ni kushuhudia majengo ya kale yenye mvuto wa kipekee.



2.Athens,Greece.
 
Athens ni mji mkuu wa Ugiriki unaokadiriwa kuwa na wakazi milioni 3. Ni mji wenye watu wanaofuata imani za kiromani,Ottoman na Byzantine.

Ni mji unaoaminika kutoa philosophers,waandishi, dramastics na wasanii wengi na nguli zaidi duniani, sifa inayoufanya kuwa wenye sifa za kipekee kabisa.

Ni mji wa kihistoria ambao una muonekano wa juu(High city), kutokana na kuwa umejengwa kwenye miinuko inayofanya kuwa na muono mzuri kuangalia chini.

Kutokana na mji huu kutambulishwa kuwa ni archeological research center, umesheheni makumbusho ya kihistoria kama National archaeological museum,The byzantine and Christian museum na The new acropolis museum.

Na kama ukifanikiwa kutembelea Athens, basi usithubutu kutotembelea bandari ya Piraeus ambayo ni bandari muhimu huko Mediterranean kwa karne nyingi zilizopita kutokana na eneo lake lilivyo kijiografia.



3.Byblos,Lebanon.
Ni mji wa zamani katika nchi ya Lebanon, na unashikilia nafasi ya tatu kwa ukubwa kwa kuwa mji mkongwe zaidi duniani ukikadiriwa kuwepo kwa zaidi ya miaka 5000. Na cha kufurahisha zaidi ni kwamba neon la kiingereza Bible likimaanisha biblia limetoholewa kutokana na jina la mjii huu,Byblos. Ni mji lovely kwa utalii.

Siku hizi umekuwa ni mji wa kisasa ukiwa na majengo ya kioo, kitu kinachoufanya uvutie zaidi kutokana na muunganiko wa utamaduni na usasa.(Traditions meets moderm).



4.Jerusalem, Israel.
Ndio mji unaotembelewa zaidi nchini Israel na vilevile ni kituo muhimu cha kidini duniani. Jerusalem ni mji unaojulikana kama ni mji mtakatifu kwa wayahudi, wakristo na waislamu. Kwa mujibu wa biblia, mji wa Jerusalem ulifanywa kuwa mji mkuu wa Israel na Daudi.

Siku hizi Jerusalem una wakazi wanaokadiriwa kufikia 800,000 huku wayahudi wakiwa wengi zaidi, wakikadiriwa kufikia asilimia 60 ya wakazi wote wa mji huo.

Ni mji ulioanzishwa miaka 4000 iliyopita na umegawanywa katika vipande vine ambavyo ni sehemu ya wakristo,waislamu,waarmenia na wayahudi, hali inayoufanya kuwa ni mji unaokumbwa na machafuko ya mara kwa mara na mashambuliza ya kujitoa muhanga kutokana na matabaka hayo, hali iliyofanya mwaka 1981 kuwekwa kwenye orodha ya mji wa urithi wa dunia uliopo katika hatari.


5.Varanasi,India.
Mji wa kiroho wa Varanasi, unapatikana kandokando ya kingo za mto Ganges na umejumuishwa katika orodha ya miji ya kale zaidi duniani. Wahindi wanaamini kuwa ni mji ulioasisiwa na mungu Shiva katika karne ya 12.BC.



6.Chochula,Mexico.
Ukiwa na zaidi ya umri wa miaka 2500, mji wa Chochula umejengeka kutoka katika muunganiko wa vijiji mbalimbali kama Olmecs,Tolteas na Azteas na unakadiriwa kuwa na wakazi elfu 60.
Chochula maana yake ni "place of flight", na hapo awali ulijulikana kama Acholollan.

Kivutio kikubwa katika mji huu ni "Great pyramid of Chochula ambayo inajulikana kama mnara mkubwa zaidi kuwahi kutengenezwa na binadamu. Ni mnara unaojumuisha njia mbalimbali chini ya ardhi na mapango yenye urefu wa kilometa 8.

7.Jericho,Palestina.
Unakadiriwa kuwa na umri wa miaka elfu kumi na moja na kukadiriwa kuwa na wakazi elfu 20.
Katika kitabu Hebrania katika biblia, mji huu unatambulishwa kama,"A city of palm trees."

Mji wa Jericho unapatikana katikati ya palestina na hivyo kuwa ni mji kiungo muhimu kubiashara.
Katika karne ya 20, mamlaka ya Jericho yalikuwa chini ya utawala wa Jordan na Israel.Mwaka 1994 mamlaka yalihama na kuwa ya Palestina.

Vivutio vikuu vya Jericho vinajumuisha Tell es Sultan, Hisham's palece na Shalom al Yisrael Synagogue Masaic floor.

8.Allepo, Syria.
Ni mji mkubwa zaidi nchini Syria ukikadiriwa kuwa na wakazi wanaofikia milioni mbili. Ni mji wenye faida sana kijiografia kwani unapakana na barabara ya Silk ambayo ndiyo inayounganisha Asia na eneo la Mediterranean.

Ni mji unaodaiwa kuwepo kwa miaka 8000 iliyopita na unajulikana pia kwa jina la "The soul of Syria."

9.Plovdiv,Bulgaria.
Ni mji unaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 4000 B.C. Kwa karne nyingi mji wa Plovdiv umekuwa chini ya tawala mbalimbali, ingawa kiuhalisia hapo mwanzoni ulikuwa mji wa Thracian. Baadaye walitawaliwa na Romans.

Katika zama za kati,Plovdiv walikuwa chini ya utawala wa Bulgaria,Byzantine na Ottoman. Lakini mwaka 1885 ndio hasa mji huu ukawa rasmi sehemu ya Bulgaria, na kuwa mji wa pili kwa ukubwa nchini humo.

10.Luoyang,China.
Mji wa Luoyang unatajwa kuwa na umri wa miaka 4000 B.C huku ukiwa na wakazi wanaokadiriwa kufikia milioni saba.

Wakati miji mingi mikongwe duniani inaonekana kupatikana zaidi Mediterranean, Luoyang unasimama kama mji mkongwe unaopatikana Asia. Ni kati ya mji uliojumuishwa katika Seven Great Ancient Capitals of China.

Mji wa Luoyang una mengi ya kujivunia lakini mojawapo ni The longmen Grottoes, ambayo ilitajwa kama eneo la urithi wa dunia mnamo mwaka 2000. Na pia mahekalu mbalimbali ya Buddhist yameufanya mji wa Luoyang kuwa kivutio kikubwa watalii kutoka duniani kote.

Luoyang pia ni maarufu kutokana na White horse temple, ambayo ni temple ya kwanza kuanzishwa nchini China.