LOGO

LOGO

Friday 19 June 2015

Tujikumbushe:Beef ya Hip Hop kati ya West Coast na East Coast.

Historia ya uhasama wa makundi ya hipo hop kutoka East Coast na West Coast!
Ni uhasama uliokuwa gumzo kubwa duniani katika miaka ya 1990's baina ya wasanii na mashabiki wa Hip Hop kutoka kambi mbili za East Coast na West Coast nchini marekani. Inazungumzwa kuwa chanzo kikuu cha uhasama wa pwani hizo mbili ni Rapper kutoka East Coast, Notorious BIG (Akiwa chini ya lebel yake kutoka jiji la New York,Bad bor records), na rapper kutoka West Coast namzungumzia Tupac(Akiwa chini ya lebel yake kutoka jiji la Los Angeles, Death row records), ambao wote walikuja kuuwawa na wauaji bado hawajajulikana. Tupac aliuawa mwaka 1996 na Notorious BIG, mwaka 1997.
 
Tupac

Notorius B.I.G
 

Hip Hop kama Hip Hop Kwa ufupi.
Hip hop ilianza katika miaka ya 1970's katika mitaa ya south Bronx. Ikipewa nguvu na Madj kama Dj Herc, Grandmaster flesh na Afrika bambataa. Aina hii ya muziki ilikuja kuwa maarufu katika kila kona ya Bronx.

Dj Herc. 

Grand masterflash 

Afrika Bambaataa

Maeneo yote ya New York yalibaki kuwa ndio kioo cha music wa Rap katika miaka yote ya 80's ambako ndipo makazi ya mastaa mbalimbali wa Rap kama Run DMC. LL Cool J, KRS One, Dougie Fresh,Rakim,Big Daddy kane, Biz Markie, Slick Rick, Salt N Pepper na wengineo.

Katika miaka ya mwanzo ya 90's Hip Hop ilifanya kazi kubwa na kuwa sauti ya watu weusi kuongelea matatizo yao kutokana na mtindo au aina ya mashairi yaliyokuwa yakiandikwa. Na kadri muda ulivyozidi kwenda Hip hop na Gangstar rap ziligeuka kuwa kuwa ndio nyenzo za kushindana baina ya Records lebels na makundi ya Kigangstar. Records lebels zilitaka kujenga heshima ili kutaka kufanikiwa kibiashara na kupata biashara kupitia biashara ya music.

Kuibuka kwa West Coast.
Akivutiwa na Rapper kutoka Philadelphia aitwayr Schoolly D, mwaka 1986, Rapper kutokea eneo lijulikanalo kama Crenshaw, Ice T, aliachia wimbo ulioitwa "6 in the morning". Inasemwa na wengi kwamba wimbo huo ndio Gangstar rap song ya kwanza kabisa kwani baada ya wimbo huo ndio Gangstar rap ililipuka na kuchanua.
 
Ice T

Kijana mmoja Erick wright, ambaye alikuwa akijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya aliona fursa ya faida na umaarufu ya Hip hop. Kwa hiyo alianza kurekodi nyimbo katika studio ndogo iliyokuwa katika garage ya wazazi wake nyumbani kwao.
Erick wright. A.K.A Eazy E

Erick wright ambaye kwa jina la kisanii anajulikana kama Eazy E, aliungana na wasanii wengine Dr.Dre, Ice Cube,Dj Yella na Arabian prince, na kwa pamoja walianzisha kundi lililoitwa N.W.A(Niggers With Attitudes). Kwa msaada wa rafiki yake aliyeitwa Jerry heller, tarehe 3 March 1987, Easy E alianzisha Studio ya kurekodia music iliyoitwa Ruthless Records, na muda mfupi kundi lao liliachia EP iliyoitwa Panic Zone ambayo ilikuwa na nyimbo kama "8 Ball" ya Eazy E na "Dope Man" ya Ice Cube.
Dr.Dre

Ice Cube 

Dj Yella.
Kutokana na kupishana katika masuala ya fedha, Arabian Prince alijitoa N.W.A muda mfupi kabla hawajatoa albamu yao iliyowapa mafanikio makubwa ya "Straight outta Compton", huku nafasi ya Arabian prince ikichukuliwa na Rapper Mc Ren. Albamu hiyo ilibebwa kiasi kikubwa na single "Fuck the Police na "Gangsta Gangsta". Ni albam iliyoitambulisha aina ya music wa hip hop na kusimika rasmi uwepo wa West Coast kwenye dunia ya Rap Music.

Arabian Prince.

Masuala ya fedha yaliua group hili. Eazy E akabaki kuwa mmiliki wa Ruthless Records, Ice cube akawa msanii wa kujitegemea na kuachia albam mbili zilizofanikiwa sana za Amerikkka's most wanted na Death certificate, huku Dr Dre akiungana na Suge knight na kwa pamoja wakawa wamiliki wa Death Row records.

Akiwa Death row records, Dr Dre aliachia albamu ambayo inaaminika ndio albamu iliyoinfluence zaidi Hip Hop duniani iliyoitwa The Chronic. Mastaa wengine waliokuwa chini ya Death row records, walikuwa ni Snoop Dog, Warren G, The lady Rage, Nate Dog, Daz Dillinger na Kurupt waliounda The Dog pound. Hadi kufikia miaka ya 90, West coast ilijipambanua yenyewe kama watawala wa Hip Hop.

Kuibuka kwa East Coast.
Mwezi April 1994, kijana wa miaka 20 kutokea mji wa Qeens, aliyejulikana kama Nassir Jones almaarufu kama NAS, aliachia albamu iliyoitwa Illmatic. Ni albamu iliyokuwa na nyimbo kumi yenye midundo simple na mashairi simple. Kuachiwa kwa albamu hii ilikuwa ni mapinduzi muhimu ya kuirudisha uhai wa East coast, kusaidia kitu kilichoitwa East Coast renaissance.(Kuchipuka upya kwa East Coast.)
Nas

Miezi kadhaa baadaye, Rapper mwingine kutoka New York alirekodi moja ya albamu ya hali ya juu duniani. Naye ni Notorius BIG, akiwa na umri wa miaka 22. Albamu iliitwa Ready to die, na ilipatiwa cheti cha gold ndani ya miezi miwili tu toka iachiwe na kusaidia Bad boy records kuonekana kwenye ramani, ikifuatia mafanikio ya albamu ya Craig mack,  "Flava in ya ear", na pia kufuatia mafanikio ya The Wu Tang Clan.

Craig Mack 
Wu Tang Clan

UGOMVI: West Coast na East Coast, nini chanzo?
1:Bad Boy Records VS Death Row Records.
Mwaka 1993, Puffy Daddy alianzisha Hip Hop lebel iliyokuwa New York, ikijulikana kama Bad Boy Records. Mwaka uliofuatia yaani 1994, Bad Boy Records iliachia alnabu mbili kutoka kwa Notorius BIG na rapper kutoka Long Island aliyeitwa Craig Mack, albamu ambazo zilifanikiwa sana kibiashara.

Ghafla aliibuka rapper mmoja kutoka California aliyeitwa Tupac Shakur alidai kuwa kulitokea tukio la uporaji na yeye alipigwa risasi 5 akiwa Quad Recording studios huko mjini Manhattan, tarehe 30 Novemba 1994, na hadharani alidai kuwa waliohusika katika tukio hilo ni Notorius BIG, Andre Harrell na Puffy Daddy.

Siku chache baada tukio hilo la kupigwa risasi Tupac na tuhuma alizozitoa, single iliyoitwa "Who shot ya" kutoka kwa Notorius BIG ilitoka hewani na kuleta hisia kwamba single hiyo ililenga kumjibu Tupac kutokana na tuhuma alizotoa ingawa Puffy Daddy na Notorius BIG walipinga wakisema single hiyo ilikuwa imesharekodiwa kabla hata ya tukio la kupigwa risasi Tupac.

Mwezi August 1995, Suge knight, bosi wa Death row records aliongea maneno haya akiwa anahutubia kwenye hafla ya utoaji wa tuzo za Source.(Source Awards). "Any artist out there that want to be an artist and stay a star, and don't have to worry about the executive producer trying to be all in the videos...all the records...dancing,come to death row." (Akimaanisha msanii yeyote ambaye anataka kuwa msanii na kubaki kuwa staa, ambaye hatohofia bosi wa lebel yake kujaribu kutokea katika video zake zote, kutokea katika nyimbo zake zote akicheza, basi anatakiwa ahamie Death row.) Maneno hayo moja kwa moja yalionekana kumlenga Puffy Daddy kwani ni kweli ana tabia hiyo ya kutokea katika video za wasanii walio chini yake hata kama hajaimba kitu huku akicheza. Ni dongo ambalo sio tu lilimlenga Puffy daddy bali lilichukuliwa kama tusi kwa wasanii wote wa Hip hop wa East coast.

Siku hiyo hiyo baadaye, uhasama ulizidi kutanuka kati ya East Coast na West Coast wakati Suge knight alipohudhuria party moja iliyoandaliwa na Jermine Dupri huko Atlanta. Wakati Party ikiendelea, rafiki wa karibu wa Suge knight aliyeitwa Jake Robles alipigwa risasi hapo hapo kwenye party. Suge knight bila kupepesa macho alimtuhumu moja kwa moja Puffy daddy ambaye naye alikuwemo kwenye party hiyo kuwa kwa namna moja au nyingine alihusika katika ufyatuaji risasi huo.
 
Suge Knight

Puffy Daddy

Mwaka huo huo Tupac alitupwa jela kwa kosa la udhalilishaji wa kijinsia na Suge knight alikwenda kumdhamini kwa kiasi cha dola 1.4 milioni ili aachiwe kutoka jela kwa makubaliano kuwa akiachiwa tu basi asaini mkataba wa kuwa chini ya Death Row Records. Baada ya Tupac kuachiwa kweli alitimiza makubaliano hayo kwa kusaini mkataba jambo lililozidisha uhasama kati ya Death Row Records na Bad Boy Records kwani tayari Tupac alikuwa na uhasama na Puffy dady na Notorius BIG kwa kuwatuhumu walimpiga risasi 5 kwenye tukiola uporaji huko Quad recording studios, Manhattan, tarehe 30 Novemba 1994.

2:Tupac VS Notorius BIG.
Kwenye wimbo wa Notorius wa "Who shot ya", kuna mstari unasema, "Come here..come here...open your fucking mouth...Didn't I tell you not to fuck with me?...cant talk with a gun in your mouth huh? Bitch ass nigga,what.(Kwa kifupi ilitafsiriwa kwamba alikuwa akimuimbia Tupac kuhusu tukio la kupigwa risasi kwake.)

Notorious B.I.G

Katika wimbo wa Tupac, "Hit em up", kuna mstari unasema, "who shot me, but punks didn't finish now you are about to feel the wrath of a manace nigga. I hit em up!"(Unaweza ukaona ni mistari ilikaa wazi kama jibu la moja kwa moja kwa nyimbo ya "who shot ya".)

Miaka ya mwishoni 1995 mpaka mwanzoni 1996 Tupac alitoa mfululizo wa nyimbo nyingi zikimlenga kumtukana, kumtishia na kumdhalilisha Notorious BIG, Bad boy records na wasanii wote waliokuwa chini ya lebel hiyo. Mfano nyimbo kama "Against all odds", "Bomb first" na "Hit em up".
Tupac

Notorious BIG naye hakuwa nyuma kwani aliachia nyimbo iliyoitwa, "Long kiss goodnight" ambayo mashairi yake yalionekana kumlenga Tupac na hata memba mmoja wa Bad Boy Records aitwaye Lil cease akihojiwa na XXL magazine alikiri kuwa nyimbo hiyo ilimlenga Tupac ingawa bosi wa Bad boy, puffy daddy, alikanusha mara moja akisema nyimbo hiyo haikumlenga Tupac, na kudai kama Notorious akitaka kumuimba Tupac basi atamtaja kwa jina moja kwa moja sio kuuma maneno.

Katika kipindi hicho vyombo vya habari viliripoti sana matukio haya na kwa kiasi kikubwa vilishiriki kuzidi kuchochea uhasama zaidi baina ya pande hizo mbili na hivyo kusababisha sasa hadi mtaani mashabiki kujitenga kwa kuchagua upande wa kushabikia hivyo uhasama ukahamia pia kwa mashabiki.

Tarehe 13 Septemba 1996, Tupac alifariki dunia baada ya kushambuliwa kwa risasi akiwa kwenye gari siku sita nyuma, alipokuwa akitoka kuangalia pambano la ngumi la Mike Tyson, huko Las Vegas, Nevada.

Mwandishi mmoja aitwaye Chuck Philips aliandika kwenye makala moja iliyokuwa na kichwa cha habari,"Who killed Tupac Shakur", kuwa shambulio hilo lilifanywa na kundi moja la kihuni la Compton lijulikanalo kama South side crips, kulipiza kisasi cha mwenzao mmoja ambaye alipigwa na Tupac masaa kadhaa nyumba kabla ya shambulio hilo. Memba huyo aliyejulikana kama Orlando Anderson alikamatwa na polisi wa Las vegas na kuhojiwa mara moja tu kabla ya kuachiwa huru. Siku chache tu baada ya kuachiwa huru, Orlando Anderson aliuawa kwa risasi katika mapigano ya makundi mawili ya kihuni.(Inahisiwa hilo kundi jingine likuwa supporters wa Tupac, ni kama walienda kulipa kisasi na wao).
Chuck Phillips

Orlando Anderson

Miezi sita baada ya kifo cha Tupac, tarehe 9 Machi 1997, Notorious BIG naye aliuawa kwa risasi huku muuaji akiwa hajulikani huko Los angeles. Mpaka leo hii mauaji hayo yamebaki kuwa hayajulikani kuwa yamefanywa na nani, ingawa wengi wanaamini Suge knight anahusika kutokana na mlolongo wa matukio ulivyo.
Baada ya vifo hivyo, uhasama nao ukaoungua kwa kiasi kikubwa kama sio kwisha kabisa.

Thursday 18 June 2015

Watu maarufu duniani waliojifungua watoto baada ya kufikisha umri wa miaka 40 na zaidi!

Imekuwa ni kama si jambo la kawaida sana kuona mwanamke ameshika ujauzito akiwa na umri mkubwa, kwa mfano kuanzia miaka arobaini. Hii inasababishwa na sababu mbalimbali lakini sababu kubwa zikitajwa kuwa ni za kiafya zaidi kwani mara zote wataalamu wa afya au madaktari wamekuwa wakitahadharisha kuwa uzazi katika umri mkubwa si salama sana na mara nyingi hushauri kama umri umeshakutupa mkono basi jitahidi usishike ujauzito. Lakini hapa ninakuletea list ya watu maarufu duniani ambao wao hawakulizingatia hilo na walishika ujauzito na kufanikiwa kupata watoto. 

1.Gwen Stefan.
Gwen Stefan alikuwa ana miaka 44 wakati anajifungua motto wake anayeitwa Apollo Bowie Flyinn, kujumuika na watangulizi wengine wa kiume aliowapata katika umri wa 30's ambao ni Kingston na Zuma.

2.Rachel Zoe.
Rachel Zoe alikuwa ana miaka 42 wakati anatangaza kwamba anategemea mtoto wa pili pamoja na mumewe Rodger Berman.

.3.Halle Berry
Super diva Halle berry alikuwa ana miaka 41 alipopata mtoto wake wa kwanza binti aitwaye Nahla Ariela Aubry, mwezi Machi 2008. Kutokana na maneno yasemwayo kuhusu ujauzito katika umri mkubwa, Halle berry alisema,"Mimba yangu ilikuwa ya ajabu sana. Nilikuwa nina furaha muda wote, nilikuwa najisikia vyema muda wote, nilikuwa nina nguvu. Nilikuwa kama superwoman. Natamani ningekuwa najisikia kama vile katika maisha yangu yote." Na kwa kuthibitisha maneno yake hayo, Halle berry alipata mtoto wa pili aitwaye Maceo wakati akiwa na umri wa miaka 47.

4.Kelly Preston.
Baada ya kumpoteza mtoto wao wa kiume,Tett, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 16, Kelly Preston na mumewe John Travolta waligubikwa upya na furaha wakati Kelly Preston alipojifungua bila matatizo yoyote mtoto wa kiume waliyempa jina la Benjamin, mwaka 2010, akiwa katika umri wa miaka 48.
Akiongea na kipindi cha televisheni cha Today show muda mfupi baada ya kujifungua kutokana na hatari ya kujifungua katika umri mkubwa alisema,"Sikuangalia kabisa kuhusu hatari iliyopo, pekee nilichofikiria ni ugumu utakaokuwepo wakati wa kujifungua."

5.Marcia Gay Harden.
Marcia gay harden alikuwa na miaka 44 wakati anajifungua mapacha wake, Hudson na Julitta Dee, katika ndoa yake na mumewe Thaddaeus Scheel. Lakini pamoja na ujauzito huo tayari alikuwa na binti mwingine, Eulala Grace, aliyempata akiwa na umri wa miaka 41.

6.Tina Fey.
Ni mwanadada muigizaji ambaye alipata mtoto wa pili aitwaye Penelope akiwa na umri wa miaka 41, akimfuatia wa kwanza aliyeitwa Alice.

7.Salma Hayek.
Muigizaji nyota Salma Hayek alikuwa na umri wa miaka 40 wakati alipojifungua binti yake aliyekuja kupewa jina la Valentina paloma pinault, kutoka katika ndoa yake na mumewe Francois-Henre Pinault.

8.Susan Sarandon.
Susan Sarandon alipata mtoto wake wa kwanza ambaye ni wa kike aitwaye Eva Amurri katika umri wa miaka 39. Bila watu kutarajia alipata mtoto wa pili ambaye ni wa kiume aitwaye Jack Henry, akiwa na umri wa miaka 42.Wakati watu wakidhani umri sasa umeshamtupa mkono, aliwastua kwa kuwaletea mtoto wa tatu ambaye alikuwa ni wa kiume pia aitwaye Miles Guthrie wakati alipofikisha umri wa miaka 45.

9.Kim Basinger.
Kim basinger akiwa kwenye mapenzi motomoto na mcheza sinema Alec Baldwin, walifanikiwa kupata mtoto wa kike wakati Kim Basinger akiwa na umri wa miaka 41.,

10.Brooke shields.
Brooke shields alipata mtoto wake wa kwanza binti anayeitwa Rowan Francis mwaka 2003 wakati huo akiwa na umri wa miaka 38. Miaka mitatu baadaye yaani mwaka 2006 akiwa na umri wa miaka 41, alimkaribisha duniani binti mwingine aliyempa jina la Grier.

11.Celine Dion.
Baada ya kusumbuliwa sana na masuala ya uzazi hususani kutoka kwa mimba mara kadhaa (Miscarriage), hatimaye Celine dion alipewa zawadi ya kipekee na mwenyezi Mungu kwa kujifungua watoto mapacha, Eddy na Nelson, akiwa na umri wa miaka 42 pamoja na mumewe Rene' Ange'lil.

12.Molly Ringwald.
Molly Ringwald alikuwa na miaka 41 wakati alipopata ujauzito na kujifungua watoto mapacha,Roman Stylianos na Adele Georgiana, mwaka 2009. Lakini tayari alikuwa mama wa binti aitwaye Mathilda Ereni.

13.Hellen Hunt.
Kellen Hunt alikuwa na miaka 40 wakati akijifungua binti yake aliyempa jina la Makena Lei Gordon Carnahan.

14.Geena Davis.
 
Geena Davis mwaka 2002 akiwa na umri wa miaka 46, alipata mtoto aitwaye Alizeh. Watu walimshangaa kuzaa katika umri wa miaka 46 lakini yeye akaamua kuwakomesha watu hao kwani mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 48 alijifungua tena watoto mapacha,Kian na Kaiis.

15.Meryl Streep.
Meryl streep alipata mtoto wake wa nne aitwaye Louisa Jacobson Gummer mwaka 1991 muda mfupi kabla hajatimiza umri wa miaka 42.

16.Nicole Kidman.
Nicole Kidman tayari alikuwa mama wa watoto wawili, Isabella na Conor, watoto waliowaasili yeye pamoja na mpenzi wake wa zamani Tom cruise. Lakini alikuja kupata mtoto wake wa kumzaa mwenyewe mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 40.

17.Mariah carey.
Mariah carey alipata watoto akiwa na umri wa miaka 42, mwaka 2011. Watoto mapacha,Moroccan na Monroe. Naye hapo awali alikuwa na tatizo la mimba kutoka(Miscarriage), kwa hiyo kupata mapacha hao ilikuwa Baraka kubwa kwake.

18.Marcia cross.
Katika kipindi cha ndani ya mwaka mmoja, Marcia cross alipata neema mbili kwa pamoja. Kwani alifunga ndoa mwaka 2006 na Tom Mahoney na pia February 2007 alipata watoto mapacha, Eden na Savannah, muda mfupi kabla hajatimiza umri wa miaka 45.

19.Beverly D'angelo.
Mwaka 2001 akiwa na umri wa miaka 49, Beverly D'angelo alijifungua watoto mapacha, Anton na Olivia Pacino, baba akiwa na star wa movie aitwaye Al Pacino.

20.Mira Sorvino.
Baada ya mimba iliyomsumbua sana, hatimaye Mira sorvino alijifungua mtoto wake wa tatu, Holden Paul Terry, mwezi June, mwaka 2009 akiwa na umri wa miaka 41.Hakukoma! Mwezi May, mwaka 2012 akiwa na umri wa miaka 44 alipata mtoto wake wa nne, binti Lucia. Mira Sorvino na mumewe Chris Backus tayari awali walikuwa wana watoto wawili, Johnny Christopher King na Mattea angel.

21.Cheryl Tiegs.
Cheryl Tiegs alipata mtoto wake wa kwanza, Zack, akiwa na umri wa miaka 44 kutoka kwenye ndoa na mumewe wa zamani Antony peck. Akawaacha watu midomo wazi mwaka 2000 kwa kupata mapacha na mumewe Rod Stryker, mapacha Jaden na Theo, akiwa na umri wa miaka 52!

22.Jennifer connely.
Jennifer connely alikuwa na umri wa miaka 40 wakati yeye na mume wake Paul bettany walipoongeza mtoto wa tatu Agnes lark, kuungana na kaka zake waliomtangulia, Kai na Stellan.Hiyo ilikuwa ni May 2011.

23.Mary Stuart Masterson.
Mary stuart masterson alifanya kweli kwa kupata mtoto wake wa kwanza akiwa na umri wa miaka 43, na mumewe wa  tatu, Jeremy Davidson. August 2011 walikaribisha watoto mapacha Mary Stuart Masterson akiwa na miaka 44. Kuonyesha uzazi wake aliupanga kila baada ya mwaka mmoja, October 2012, akiwa na umri wa miaka 45, akapata mtoto wa nne.

24.Uma Thurman.
Baada ya kupata watoto wawili na mume wake wa zamani Ethan hawke, ambao ni Maya na Leven, Uma Thurman alimkaribisha mwanaye wa tatu Rosalinda Arusha ArkadinaAhalune Florence Thurman-Busson, mwezi July 2012 akiwa na umri wa miaka 42.

25.Julianne moore.
Mwezi April 2002, Juliane moore alipata mtoto wake wa pili,Liv, akiwa na umri wa miaka 41. Mtoto wake wa kwanza anaitwa Caleb.

26.Naomi watts.
Naomi watts alianza kutengeneza familia yake mwaka 2007, baada ya kuzaliwa kwa mtoto Sasha wakati huo akiwa na miaka 39. Mwaka mmoja baadaye yaani December 2008, akiwa na umri wa miaka 40, aliimarisha familia yake kwa kujifungua mtoto wa kiume anayeitwa Samuel. 

Tuesday 16 June 2015

Visingizio Baada ya timu kufungwa!!

Visingizio vya kijinga zaidi kutoka kwa makocha na wachezaji!

Katika soka waandishi wa habari wanakutana na visingizio vingi kutoka kwa wachezaji na makocha wa timu mbalimbali kutokana na matukio mbalimbali ya ndani na nje ya uwanja.Hata hivyo, kuna visingizio vingine vinachekesha sana.

1.Kutoka kwa Francesco Totti na Christian Panucci.
Francesco totti.

Christian Panucci.

Mfanyakazi mbovu kila siku atalaumu zana zake. Na ndicho kilichotokea kwa mastaa wawili wa timu ya taifa ya Italia, Francesco Totti na Christian Panucci baada ya suluhu ya 0-0 dhidi ya Denmark michuano ya Euro 2004.
Totti aliamua kulaumu vikali kuhusu viatu vyake huku akidai kwamba kuvaa viatu hivyo ilikuwa ni sawa na kutumbukiza mguu wako katika mchanga unaochemka. Panucci ndiye aliyetoa kali zaidi kwa kulaumu soksi zake."Nyuzi ambazo zimetumika katika kutengeneza soksi hizi zimetengenezwa vibaya sana."
Kweli wachezaji wa kulipwa kama hawa wanaweza kutoa visingizio hivi kweli eti kuwa ndio sababu ya kutoka suluhu?

2:Kenny Dalglish.
  
Mara nyingi makocha mbalimbali duniani huwa wanalia sana na waamuzi pindi matokeo yanapokuwa yale ambayo hawayajayatarajia.Lakini wapo makocha wengine ambao huwa wanalia na uzembe wa wachezaji wao katika kutimiza majukumu yao.
Hata hivyo mwaka 1998, kocha wa New castle united, Kenny Dalglish alikuja na kisingizio tofauti kabisa ambacho hakikutegemewa na yeyote yule wakati New castle iliposhindwa kuifunga timu isiyo katika daraja lolote lile ya Stevenage Borough katika michuano ya kombe la FA. Daglish alilalamika mipira iliyokuwa inatumika katika mchezo ule ilikuwa inadunda sana, eti ndio maana wakashindwa kuifunga timu ile.

3.Yaya Toure.
 
Baada ya kumalizika kwa michuano mbalimbali msimu wa 2013-14, kiungo wa Manchester city, Yaya Toure alitoa madai ya kushangaza na ya kitoto kuwahi kutolewa na mchezaji wa aina yake.
Toure kupitia wakala wake, Dimitri seluk, alidai kwamba alikuwa anafikiria kuondoka Manchester city kwa sababu timu hiyo ilikuwa haimpendi na ilishindwa hata kumpelekea keki maalumu katika sherehe yake ya kuzaliwa alipotimiza miaka 31, Mei 13,2014.
Hivi ni kweli klabu inayokulipa mshahara wa Pauni 250,000 kwa wiki unaweza kusema inakupuuza kwa sababu tu ya kushindwa kukuletea keki?

4.Sir Alex ferguson.
Bingwa mwingine wa visingizio huyu hapa. Kwa miaka mingi ya utawala wake old traford, sir Alex erguson alikuwa analaumu vitu mbalimbali kama Manchester united ikichemsha.
Hata hivyo mwaka 1996, wakati Manchester united ilipopigwa bao nyingi na Southampton, Ferguson alikuja na kisingizio cha kuchekesha kweli kweli.
Ferguson alidai kwamba timu yake ilipoteza mechi hiyo kwa sababu ilikuwa imevaa jezi za kijivu. Akadai kwamba wachezaji wake walikuwa hawaonani vizuri uwanjani kutokana na rangi za jezi hizo.
Hata hivyo kisingizio cha Ferguson kilionekana cha uongo zaidi kwani walibadili jezi wakati wa mapumziko na bado ikafungwa mabao matatu zaidi kipindi cha pili.

5.Wayne rooney.
Yaya toure si mchezaji wa kwanza kuishawishi klabu yake kumpa mkataba mpya kwa kutumia sababu za kitoto.
Mwaka 2010, staa wa Manchester united, Wayne rooney aliripotiwa akida kwamba alikuwa anataka kuondoka klabuni hapo kwa sababu ya klabu hiyo imekosa tama ya mafanikio.
Hata hivyo, wiki moja baadaye Rooney aliongezewa mshahara wake kufikia pauni 250,000 na kelele zake zikaisha.

6.Vladislav vashchuck.
 
Katika fainali za kombe la dunia mwaka 2006 nchini ujerumani, Ukraine ilichapwa mabao 4-0 na Hispania. Wakati ikionekana kuwa labda waukraine wangeweza kukubali kichapo hicho na kukiri kwamba walikuwa wamezidiwa,kumbe beki wao,Vladislav vashchuck alikuwa na mawazo mengine kabisa.

Vashchuck alilaumu kelele za vyura waliokuwa wanalia nje ya ya hoteli waliyofikia usiku wa kuamkia siku ya mechi kwa madai waliwakosesha usingizi na hivyo kuwafanya wawe wachovu siku ya mechi.
"Kwa sababu ya vyura kupiga kelele hatukuweza kupata walau lepe la usingizi.Wote tulikubaliana tuchukue fimbo kwenda nje kuwawinda na kuwapiga." Alisema Vashchuck.

7.Jose Mourinho.
 
Orodha hii ya visigizio haiwezi kukamilishwa bila ya kuwepo kocha huyu wa kireno mwenye maneno mengi.Ni mtaalamu wa visingizio.
Mwaka 2011 alipoteza pambano la supercopa dhidi ya Barcelona iliyokuwa katika ubora wa hali ya juu sana, haikutazamiwa kuwa Mourinho aliyekuwa kocha wa Real Madrid angewapongeza Barcelona kwa sababu ni kocha mwenye majivuno mengi, lakini hata hivyo kisingizio alichotoa kilichosha wengi.
Mourinho alilalamika kwamba katika pambano hilo hakukuwa na watoto waokota mipira inapotoka nje wa kufanya kazi hiyo kwa haraka."Hakukuwa na watoto waokota mipira katika kipindi cha pili." Alilalamika Mourinho, eti ndio sababu ya wao kufungwa pambano lile.

8.Kolo Toure.
Inaonekana familia ya kina Toure ina vichekesho vya kushangaza, baada ya kufungiwa miezi sita kutokana na kufeli katika vipimo vya dawa za kuongeza nguvu, Kolo aliamua kupeleka kesi hii kwa mkewe.
Alidai kwamba dawa hizo alipewa na mkewe kwa ajili ya kupunguza uzito lakini kumbe zilikuwa na chembe chembe za dawa za kuongeza nguvu.Alitoa kauli hiyo utafikir si mchezaji wa kulipwa.

9.Crystal palace.
 
Mashabiki wa mpira ni hodari sana wa kukosoa timu zao pindi zinapofanya vibaya. Hata hivyo mnamo mwaka 2011,mashabiki wa klabu ya crystal palace, baada ya timu yao kufanya vibaya waligundua kwamba sababu  kubwa haikuwa wachezaji.
Mashabiki wa palace waliamua kuwa ni mashabiki warembo wanaoikaribisha timu hiyo uwanjani wakati wa kuingia maarufu kama cheerleaders ndio waliokuwa sababu ya timu kufungwa kwa sababu wachezaji walijikuta wakiwakodolea macho zaidi kuliko kuzingatia soka.
Shabiki mmoja alikwenda mbali kwa kusema,"wanamuondoa kila mtu mchezoni.Unaona wachezaji wanavyowaangalia wao tu wakati ambapo inabidi wazingatie mechi.Afadhali warembo hao waondolewe"

10.Adrian Bradbnam.
Moja kati ya visingizio vya kipumbavu katika soka kimojawapo ni hiki cha mshambuliaji wa wa klabu ya Sutton united, Adrian bradnam, ambaye aliwahi kulaumiwa kwa kukosa bao la wazi kabisa akitizamana na nyavu.
Bradnam alijibu mapigo kwa kudai alikosa bao hilo kutokana na kelele nyingi za mashabiki uwanjani hapo. Hivi mchezaji wa kulipwa unategemea nini ukienda katika uwanja wa soka na katika pambano la ushindani?

Visingizio tu, noooma saaaana!!
Kwa hisani ya gazeti la mwanaspoti.