LOGO

LOGO

Tuesday 10 February 2015

Kama mkwanja upo wa kutosha, hii ndio miji ya kutembelea duniani!!

Mara nyingi watu wanapoenda mapumziko baada ya mihangaiko ya mwaka mzima, aidha kwa kwenda kutalii au kupumzika tu, basi kati ya vitu ambavyo huwa wanaviangalia sana ni baljeti ya safari nzima. Si uongo wala kificho kuwa wengi huangalia na kupanga kwenda sehemu yenye unafuu wa gharama. (Low budget destinations.)

Lakini kuna suala moja, kuna tatizo gani angalau mara moja kati ya miaka kadhaa hivi ukaamua kuchana mfuko na kuamua kula bata haswa(Pamper yourself) katika maeneo luxuries zaidi? Maana ukweli uko wazi, maeneo luxuries huwa ndio salama na mvuto wa pikee. Hebu take time one day vunja akaunti yako na ukajiachie katika miji na maeneo yafuatayo, hutojuta!

1.Monaco.
Ni mji mdogo unaopatikana kwenye pwani ya ufaransa. Monaco ni maarufu kwa film festival na vitu vitu vya gharama na anasa. Wanasema kila mtu anayeishi Monaco anataka kuishi kifalme, na wanafanya hivyo haswa bila kujinyima. Kuna majumba na magari ya kifahari, maduka ya kushangaza na migahawa ya hali ya juu inayofanya mji wa Monaco kuwa mji wa kifahari ambao kama hali yako ya kifedha inakuruhusu basi usisite kuutembelea.

Hoteli nyingi mjini Monaco ni ghali sana ingawa utapata huduma ya hali juu na utakuwa confortable kiasi kwamba hutokumbuka wala kujutia kiasi ulichotumia.

2.French Polynesia.
Ni mji unaojulikana kama Tahiti. French Polynesia ni paradise ya ukweli, iliyoko kusini mwa bahari ya pacific. Kuna bungallows ambazo ziko kwa juu milimani kuzunguka bahari na ndipo accomodations nyingi zinapopatikana kama ukitembelea sehemu hii, ambapo utapata private villas zenye mandhari nadhifu, huku ukiletewa breakfast kwenye kibaraza chako ili upate kifungua kinywa huku ukitazama mandhari ya bahari kwa chini.

Pamoja kuwa French Polynesia ni sehemu ya kufikia kwa ajili ya kurelax, lakini pia kuna vitu vingine vingi vya kuvutia vya kufanya pale, hususani kwa wapenzi wa michezo ya kwenye maji.(Water sports).

3.Dubai.
Dubai ni kati ya sehemu ambazo kila mtu anaota kupatembelea angalau maramoja katika uhai wake. Ni moja kati mji wa kuvutia duniani uliofurika majengo marefu(Sky scrapers), Hotels za hali ya juu. Na usishangae, ndio mji wenye maduka makubwa ba ghali zaidi duniani kwa ajili ya shopping. (The world's most expensive and biggest shopping malls).

Wakati nchi nyingi umezoea kusikia wana 5 star hotels, lakini Dubai inajulikana kwa kuwa na Hoteli ya nyota 7 (7 star hotel), yenye vyumba vya mpaka kifalme sio presidential suits tu, vyumba ambavyo vinafikia mpaka dola 10,000 kwa usiku mmoja.

Ni mji maarufu wa wasafiri wa kibiashara na watalii amabo wanamudu gharama za mji huu.

4.Maldives.
Ni moja ya miji mizuri sana kama unataka kwenda for honeymoon. Maldives inakumuisha visiwa mbalimbali ambavyo vyote vina mvuto wa kipekee.

Waansema watu wanaoishi hapa wanatengeneza fedha nyingi sana, na nyingi kati ya hizo zinatokana na utalii na shughuli za uvuvi. Kutokana na kipato kuwa kikubwa, ndicho kinachofanya bei za migahawa na hotels nazo ziwe juu sana pia.

5.Singapore.
Miaka michache nyuma Singapore ilikuwa ni sehemu amabayo unaweza kufikia kwa gharama za kawaida kabisa, lakini kwa kasi ya hali ya juu pamegeuka kuwa a true luxury destination. Imejenga estates, hotels za luxury, shopping malls na migahawa mingi yenye hadhi ya dunia.(World class restaurants). Inakadiriwa vyumba vya hotel za wastani ni dola 200 kwa siku. Ni sehemu nzuri kutembelea kama umejipanga kutuonea huruma mfuko wako wa fedha.

6.Japan.
Unaweza ukajiuliza na kushangaa kuona Japan imeingiaje kwenye List hii ya luxury destinations, lakini ukweli unabaki kuwa ndio huo kuwa ni mahali pa gharama kubwa kupatembelea. Ni mahali sahihi kama unataka kufanya vacation ya gharama. Hata kama utataka kufikia katika hotels za gharama ya wastani, bado itabidi uwe na si chini ya dola 250 kwa usiku mmoja.

Kuna vitu vingi vya kufanya ukiwa Japan, so sio sehemu ambayo utakuwa boered. Kuna miji mingi yenye uzuri wa kushangaza, mambo mengi matamu ya utamaduni, fukwe za kuvuti na mandhari adimu za milima.

Usihofu kama hujui kuzungumza Kijapani, utatumia ishara za mikono tu kuwasiliana na wenyeji, maana hawa jamaa wengi wao hawajui kiingereza!!!

7.Fiji.
Fiji ni maarufu kwa kutembelewa na wageni kutoka Australia, New Zealand na marekani. Pamoja na Fiji kuwa mara zote imejaza watalii, lakini siku zote imekuwa ni sehemu ya amani, huku shughuli za honeymoon zikiwa ndio mahala pake haswaa.

Ina milima miangavu ya kijani, fukwe za michanga myeupe(White sandy beaches). Hoteli zake ni za kisasa na luxury haswa, pia ziko romantic na kuna mengi ya kufanya hususani ukiwa mpenzi wa michezo ya kwenye maji.

Na kama unataka kujifunza mambo ya utamaduni, basi usiache kutembelea baadhi ya vijiji hapo Fiji, utafurahi.

Fiji ina shughuli nyingi za kustaajabisha(Adventure activities), zitkazokustua na kumvutia kila mtu atakayebahatika kufika pale!!

No comments:

Post a Comment