LOGO

LOGO

Monday 9 February 2015

Unajua kwa nini Jokate anapapatikiwa na wanaume? Mwenyewe aelezea....

Ni mshindi wa miss Temeke mwaka 2006, ushindi uliompa Ticket ya kushiriki Miss Tanzania ingawa hakubahatika kuwa mshindi, alishika nafasi ya pili, ila alifanikiwa kuutwaa ubalozi wa bia ya Redds. Hapa namzungumzia Jokate Mwegelo....

Pamoja na kutoshinda taji la Miss Tanzania mwaka huo lakini kushiriki kwake tu ilikuwa kama ndio mlango umefunguliwa wa mafanikio katika Nyanja nyingine. Kwani baada ya hapo aligeukia filamu akiigiza movie kama fake pastors na chumo, akaingia kwenye music na kufanya vizuri ingawa sio sana.


Akaingia pia kwenye suala la endeshaji shughuli, "msema chochote", shughuli za U-Mc. Hapa amefanikiwa sana kwani amefanikiwa kuongoza shughuli nyingi kubwa za tuzo au sherehe mbalimbali na hivyo kujiingizia mkwanja wa kutosha.


Kubwa jingine lenye mafanikio ni suala la mitindo, ameshika sana eneo hili. Unapomzungumzia Jokate na mitindo basi lazima uzungumzie Kidoti. Kidoti ni brand ya mitindo inayomilikiwa na Jokate mwenyewe. Humo utakutana na nywele, mavazi na sandals. Kidoti ni brand inayozidi kumfungulia njia ya mafanikio kimataifa, kiasi cha kupata deal na wachina, deal lililomuingizia billions of money, sizungumzii milioni hapa, ni billions.


Upande wa modeling naye yumo, mara kwa mara amekuwa akionekana kwenye matukio mbalimbali akifanya catwalks na vitu kama hivyo. Mfano alishawahi kushiriki onesho la mitindo la Red Ribbon lililokuwa maalumu kwa kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto walioathirika na ugonjwa wa ukimwi chini ya taasisi T anzania mitindo house iliyo chini ya mwenyekiti, Khadija mwanamboka.

Lakini pia ni mtangazaji wa TV kitaifa na kimataifa. Kitaifa amefanya kazi na TV1 wakati kimataifa ametusua mpaka pande za kwa mzee madiba na kufanya kazi na kituo bora kabisa cha televisheni duniani, channel O.


Anyway yote kwa yote amewahi kuzungumzia kidogo kuhusu suala la mapenzi. Aliongelea tu kwa nini wanaume wengi humpapatikia yeye?

1.Kujiamini.
Anasema hamna kitu kinachowavutia watu hasa wanaume kama kujiamini. Mwanaume anapenda msichana anayejiamini. Na yeye anasema kuwa  ni wanamke anayejiamini sana that why midume inawatoka midenda!


2.Kujitegemea.
Anasema hii nayo inafanana na suala la kujiamini. Anasema hamna kitu kinachowaboa wanaume kama kuwa na mwanamke ambaye anapenda vitu vya kupewa. Ukimuonesha mwanaume kuwa wewe unapenda kutafuta vya kwako basi jua atakupenda sana.


3.Kupendeza.
Jokate anasema ni muhimu kwa wadada kuvaa nguo nzuri ambazo zitakupendeza kulingana na mwili wako hasa nguo zenye rangi ya kuonekana. Hapa akitaja sila yake mojawapo ya kupendwa kuwa ni kupendeza kwake.


4.Tabasamu.
Sio kila saa unanuna tu, Tabasamu. Jokate anasema ukitabasamu kila saa, tabasamu hilo linakufanya unaonekana ni mzuri zaidi.


Kazi kwenu wadada, mwenzenu anaamini katika mambo hayo manne yanayosababisha wanaume wapigane vikumbo kwake!!

No comments:

Post a Comment